Showing posts with label Vyakulanavifaa. Show all posts
Showing posts with label Vyakulanavifaa. Show all posts

Wednesday, November 16, 2016

UANDAAJI WA CHAKULA CHA KUKU

RLDC na Uboreshaji wa Maisha Vijijini Shirika la Rural Livelihood Development Company (RLDC ni moja ya mafanikio ya ushirikaiano kati ya Tanzania na Uswisi kwenye mchakato wa kupambana na umaskini na kuboresha maisha ya jamii za vijijini. Hii ni taasisi isiyo ya kibiashara ili yoanzishwa mwaka 2005 na mashirika ya Intercooperation na Swisscontact, lengo kuu likiwa kutekeleza Programu ya kuendeleza maisha ya jamii za vijijini (RLDP). Programu hii inasha bihiana na Mkakati wa Kukuza Uchumi na Kupambana na Umaskini (MKUKUTA). Dhamira kuu ya RLDC ni Kuendeleza/kuboresha mifu mo ya masoko ili kuwawezesha wazalishaji wa vijijini kutumia fursa zilipo kuboresha maisha yao. Kwa sasa, RLDC inatelekeleza awamu ya pili ya mpango wake (2008-2011) na inaweka msukumo zaidi kwenye uendelezaji wa mifumo ya masoko. RLDC inafanya kazi katika mikoa sita ya Kanda ya kati-Dodoma, Singida, Morogoro, Shinyanga, Tabora, na Manyara. Jamii nyingi maskini zinaishi katika ukanda huu wenye sehemu kubwa yenye hali ya mvua chache na nusu jangwa inayostawisha shughuli chache za kiuchumi. Hata hivyo kuna fursa nyingi sana zinazoweza kutoa ajira na kuboresha ya jamii zake. RLDC inafadhiliwa na Serikali ya Uswisi kupitia shirika la Uswisi la maendeleo (SDC). Kwa sasa RLDC inawezesha sekta za pamba, alizeti, maziwa, ufugaji wa kuku wa kienyeji, mpunga na habari kupitia vipindi vya redio kwa ajili ya wazalishaji wa vijijini. “RLDC inaboresha mifumo ya masoko ili kuwezesha wazalishaji wa vijijini kuinua maisha yao”




Thursday, August 11, 2016

UTAJIRI KATIKA MIRADI YA KUFUGA KUKU


UTAJIRI KATIKA MIRADI YA KUFUGA KUKU
Mradi wa kufuga kuku ni mradi ambao huleta faida kwa muda mfupi sana.
Ili upate faida kubwa ni vizuri ukawa na mradi ambao unaweza kuumudu kwa kuwa na mahitaji muhimu katika mradi wako.

MFANO, mtu anayetaka kufuga kuku tuseme 500 anatakiwa kuwa na vifaranga 550. Awe ana uwezo wa kuwalisha hao vifaranga na kuwapa tiba. Pia awe na uwezo wa kujenga banda bora.

 Baada ya hapo kinachotakiwa ni umakini wa kufuatilia mradi katika kipengele cha utoaji huduma kwa kuku hao. Katika kundi hilo la kuku 500, 50 wanatakiwa kuwa majogoo na 450 mitetea.
Katika hao mitetea 450 aslimia 75 wanatakiwa watage kila siku. Asilimia 75 ya 450 ni kuku 337. 

Mayai ya kuku hawa huuzwa kwa Tsh. 300@. Hivyo kila siku utapata Tsh 337 x 300 = Tsh. 100000.

Kama mtu anaweza kupata Tsh. 100000 kila siku kwa mwezi una uhakika angalau wa kuweka akiba ya Tsh. 100000 bila shida. Kama utaweka akiba ya fedha hiyo kila mwezi bila shida kwa mwaka utakuwa umeweka akiba ya shilingi milioni kumi na mbili.

Watu wengi wanaweza kufikiri hii ni nadharia ambayo haiwezekani, UKweli ni kuwa hiki kitu kinawezekana bila shida kabisa.

Ikiwa utahitahiji usaidizi njoo kwetu tukuelekeze namna unavyoweza kuondokana na umaskini usio wa lazima.

Kumbukeni ndugu wajasiriamali kwamba ukiamua ni kweli ndoto yako itatimia.