RLDC na Uboreshaji wa Maisha Vijijini
Shirika la Rural Livelihood Development Company (RLDC ni moja ya mafanikio
ya ushirikaiano kati ya Tanzania na Uswisi kwenye mchakato wa kupambana na
umaskini na kuboresha maisha ya jamii za vijijini. Hii ni taasisi isiyo ya kibiashara
ili yoanzishwa mwaka 2005 na mashirika ya Intercooperation na Swisscontact,
lengo kuu likiwa kutekeleza Programu ya kuendeleza maisha ya jamii za vijijini
(RLDP). Programu hii inasha bihiana na Mkakati wa Kukuza Uchumi na Kupambana
na Umaskini (MKUKUTA). Dhamira kuu ya RLDC ni Kuendeleza/kuboresha mifu
mo ya masoko ili kuwawezesha wazalishaji wa vijijini kutumia
fursa zilipo kuboresha maisha yao.
Kwa sasa, RLDC inatelekeleza awamu ya pili ya mpango wake (2008-2011)
na inaweka msukumo zaidi kwenye uendelezaji wa mifumo ya masoko. RLDC
inafanya kazi katika mikoa sita ya Kanda ya kati-Dodoma, Singida, Morogoro,
Shinyanga, Tabora, na Manyara. Jamii nyingi maskini zinaishi katika ukanda huu
wenye sehemu kubwa yenye hali ya mvua chache na nusu jangwa inayostawisha
shughuli chache za kiuchumi.
Hata hivyo kuna fursa nyingi sana zinazoweza kutoa ajira na kuboresha ya
jamii zake. RLDC inafadhiliwa na Serikali ya Uswisi kupitia shirika la Uswisi la
maendeleo (SDC).
Kwa sasa RLDC inawezesha sekta za pamba, alizeti, maziwa, ufugaji wa kuku wa
kienyeji, mpunga na habari kupitia vipindi vya redio kwa ajili ya wazalishaji wa
vijijini.
“RLDC inaboresha mifumo ya masoko ili kuwezesha wazalishaji wa
vijijini kuinua maisha yao”
No comments:
Post a Comment