Thursday, August 11, 2016

MAGONJWA NA TIBA YAKE




habari za wakati huu wapendwa wafugaji na wasio wafugaji,wasomi wamachapisho yetu kwa ujumla.katika toleo hili tunachambua magonjwambalimbali ya kuku.magonjwa ya kuku husabibishwa na vitu mbali mbaliikiwemo virusi,minyoo,bakteria,uchafu,wadudu na hata upungufu wavirutubisho katika vyakula vya kuku hawa.magonjwa ambayo husababishwana virusi hua ni vigumu sana kutibika hivyo mfugaji hushauliwa kuwapachanjo ya magonjwa hayo.mfano ni mdondo(new castle disease).ugonjwahuu ni hatari sana kwa kua humaliza kuku wengi kwa wakati mmoja.wenginehuita huu ugonjwa kideri.
   Mdondo(new castle disease). 
kama binadamu aogopavyo ugonjwa wa UKIMWI,basi wafugaji wengihuogopa sana ugonjwa wa mdondo,pia huitwa kideli(newcastle disease).huuni ugonjwa HATARI unaosababishwa na virusi pia ni ugonjwa huu haunatiba.Hivyo mfugaji anatakiwa kuwapa chanjo mapema kabla ugonjwahaujafika eneo hilo.dalili za mdondo ni kama.
1.kuku kukohoa au kuhema kwa tabu 
2.manyoya ya kuku huvurugika na kua katika hali isiyo ya kawaida.
3.kuku huarisha kinyesi cha kijani
3.kupoteza hamu ya kula na mabawa kupoza
4.kizunguzungu na kuanguka chali
5.kupoteza fahamu 

ugonjwa huu hupelekea kuku wengi kufa kufikia hadi asilimia 50 hadi 100 kama usipo dhibitiwa mapema.
Namna ya ugonjwa unavyosambaa
1.virusi hawa huweza kusambaa kwa njia ya hewa au upepo husafirishavirusi hawa.
2.kinyesi cha kuku mwenye mdondo kikikanyagwa na mtu,baiskeli auwanyama wengine na kusafirishwa kwenye banda la kuku,ugonjwa huuhuweza pia kusambaa.
3.kuku alie kufa kwa mdondo asipo zikwa vizuri au kuchomwa moto,kukumzima akila mabaki hayo,kuku hao watakua katika hatari ya kupata mdondo.
JINSI YA KUPAMBANA NA MDONDO
Kama ilivyo elezwa hapo juu,gonjwa hili halina tiba.lakini kuku wakipewachanjo kwa wakati hua katika usalama.kuna chanjo kama;
1.LASOTA
chanjo hii ni ya vidonge,kidonge kimoja huchanganjwa na maji safi.chanjo hiitolewa baada ya siku tatu kisha rudi baada ya wiki tatu  na rudia kila baadaya majuma manne au kutokana na uonavyo.kabla ya kuku kupewa dawa hiiyapaswa wasipewe maji kwa masaa kadhaa kwa siku hio na muda wa kupewa maji basi wapewe sehemu yenye kivuli.
chanjo hii hupatikana katika maduka mbali mbali ya mifugo.
2.Chanjo ya Thermostable 1-2,dawa hii inahuwezo mkubwa wa kustahimili joto,watu wasio na majokofu basi tumia dawa hii ila hifadhi sehem kavu na isio na joto.dawa  hii huweza kukaa wiki mbili baada ya kufunguliwa kwa Mara ya kwanza.
EPUKA YAFUATAYO
kununua kuku katika minada na kuleta bandani 
kuruhusu kila mtu kuingia katika banda la kuku
kuacha mabaki ya kuku walikufa ovyo katika mazingira ya kuku
pia,endapo kuku wengi walikufa katika banda hilo basi ni vyema usilete kuku wengine katika banda hilo angalau kwa ,mwezi au zaid.
Tenganisha kuku wenye dalili za ugonjwa na kuku wengine.
ZINGATIA USAFI WA BANDA NA VYOMBO VYA KUKU WAKO.

usikose kutembelea blog hii kwa taarifa nyingine zaidi kuhusu ufugaji wa kuku

MASHINE YA KUANGULIA MAYAI YA KUKU



Habari za wakati huu wafuatiliaje wa machapisho yetu.Leo tutatazamia njia kuu mbili za kutotoresha mayai ya kuku wa kienyeji,njia hizo ni kumuacha kuku kutotoa mwenyewe na kumuwekea mazingira.njia ya pili ni kwa kutumia mashine za kutotoreshea.


NJIA ASILIA
kwa kutumia njia hii kuku ataachwa kutaga,kuatamia,na kutotoa mwenywe.mfugaji aandae mabox au mfuko kisha aweke vitu vyenye kutunza joto kama mchanga au matambaa kisha mabox hayo yawekwe katika mabanda ya kuku sehemu tulivu na yenywe kivuli


kuku hugata mayai 10-14 kutegemeana na aina ya kuku.kuku huweza kutotoa mayai 8-14


NJIA YA KISASA
Baada ya kuandaa sehemu ya kuku kutagia,kusanya mayai kila siku na kuweka katika trei.Uwekaji wa mayai hayo,sehemu kubwa ya yai iwe juu na incha yake iangalie chini.Hii husaidia katika utotoleshaji kwenye mashine.mashine hutotoresha vizuri zaidi endapo mayai yatakua yalikusanywa katika kipindi kifupi kuanzia siku 1-6 na kuwekwa katika mashine (incubator)

 MASHINE YA KUTOTORESHEA VIFARANGA(INCUBATOR)
Hii ni mashine ambayo hufanya kazi ya kuatamia na kutotoa mayai.mashine ina uwezo wa kutoto mayai mengi,mashine ndogo huweza kutotoa mayai 25-50.mashine hii hutoa joto sawa na joto la tetea,inashauliwa kugeuza geuza mayai kwa siku angalau mara tatu katika mashine ili kupata mazao bora zaidi.










CHANGAMOTO YA MASHINE HII
Inahitaji utaalamu kuitumia
inahitaji muda mwingi kukaa nayo karibu
ni gharama kuiendesha.





AINA / KOO ZA KUKU




Kuna Koo nyingi za kuku wa asili zinazopatikana hapa nchini.

                                   KOO

Baadhi ya Koo hizo na sifa zake ni hizi zifuatazo:



                               1.   Kuchi: 



                            Sifa zake za Kuchi:

a)      Ana umbo lenye ukubwa wa wastani.
b)      Hana upanga kichwani.
c)      Ana mdomo mfupi.
d)     Ana shingo ndefu yenye manyoya.
e)      Ana ngozi ya rangi ya njano
f)       Ana miguu mirefu isiyo na manyoya
g)      Ana uwezo mkubwa wa kujihami
h)      Wanapatikana mikoa ya Tabora, Singida, Shinyanga, Mwanza, na Tanga.



2 Kishingo:

              Sifa zake za Kishingo:

Ø  Ana umbo lenye ukubwa wa wastani 
Ø  Ana upanga kichwani.
Ø  Ana shingo isiyo na manyoya.
Ø  Ana ngozi yenye rangi ya njano au nyeusi.
Ø  Ana miguu mifupi isiyo na manyoya.
Ø  Anapatikana mikoa yote ya Tanzania. 

                        3 Bukini:
        Sifa zake za Bukini :

Ø  Ana umbo fupi na ni mnene.
Ø  Ana upanga kichwani.
Ø  Ana shingo yenye manyoya.
Ø  Ana ngozi yenye rangi ya njano.
Ø  Hana manyoya ya mkia.
Ø  Wanapatikana kwa wingi katika mikoa ya Tanga, Pwani, Kilimanjaro, na Singida.
                                 Ana miguu mifupi isiyo na manyoya.
           o   Ana miguu mifupi isiyo na manyoya.



     4  Kinyavu / nungunungu/kuchere:

            Sifa zake Kinyavu:

Ø  Ana umbo dogo akilinganishwa na Kishingo na Kuchi
Ø  Ana shingo yenye manyoya.
Ø  Ana ngozi yenye rangi ya njano.
Ø  Ana manyoya yaliyosimama.
Ø  Ana mkia mrefu wa wastani.
Ø  Anapatikana katika mikoa yote nchini.
        5  Kawaida /Kitewe:

            Sifa zake Kawaida / Kitewe:

Ø  Ana umbo dogo ukilinganisha na Kuchi au Kishingo.
Ø  Ana shingo yenye manyoya.
Ø  Ana ngozi yenye rangi nyeupe, njano au nyeusi
Ø   Ana manyoya ya mkia yenye urefu wa wastani.
Ø  Anapatikana mikoa yote ya Tanzania.

WASIFU NA MAWASILIANO

JINA:   KAROLI ALEX

SIMU NAMBA:  0767 574 013

E-MAIL-  karolialex076@gmail.com

LOCATION OF PROJECT:  Namibu,Kibara,Bunda,Mara,Tanzania



UENDESHAJI WA MRADI WA KUKU-KIBARA

 UENDESHAJI WA MRADI WA KUKU WA MAYAI:

Iili kufanikiwa kufikia malengo ya kufuga kuku wa mayai  ni vyema mfugaji akapata wasaa wa kujiuliza maswali kadhaa ili awe na dira sahihi ya kile anachotarajia kufanya kutokana na mapato ya mradi huo.
Dira ni picha ya matokeo yanayotarajiwa yanayotokana na juhudi na maarifa .
Bila shaka kabla ya kuanza kufuga utakuwa umejiuliza ni kwa nini ufuge kuku wa mayai na wala sio kufanya kitu kingine ; swali kama hili litakusaidia kuwa na muelekeo wa kile unachotarajia na hivyo kuweka mkakati sahihi wa kusimamia mradi wako wa kuku wa mayai.Mfano , pengine umeamua kufuga kuku kwasababu kuna upatikanaji wa pembejeo kwa urahisi kama vile upatikanaji wa vifaranga, viinilishe, madawa na kubwa zaidi ni upatikanaji wa soko la mazao yako.
Vyovyote iwavyo mambo yafuatayo ni vizuri yakazingatiwa ili kupata mafanikio katika mradi wa kufuga kuku wa mayai;
1.      Uwe na uhakika wa kupata vifaranga kutoka kwa wasambazaji mahiri     ( reliable Day old Chicks breeders and Suppliers)
2.      Zingatia ratiba ya kulisha. Lisha kuku  chakula kinachopendekezwa kwa kuzingatia umri  na uzito.
3.      kagua na na fanya usafi mara kwa mara na katika nyakati zilizopangwa(inspect and carry out specificl and periodical hygienic operations)
4.      toa matunzo kwa kwa kuzingatia mahitaji ya makundi.
 
5.      Tengeza viota ili kuku waweze kutaga mayai kwa faragha bila bughudha kutoka kwa wengine. Vilevile viota husaidia kuwa na mayai safi na husaidia kuepuka kuvunja kuvunjika na kuchafuka kwa mayai mara kwa mara.
6.      Hakikisha unasafisha mayai kwa kitambaa safi  baada ya kuokota na kabla kuwauzia wateja.
7.      Zingatia matakwa ya wateja kwa kuainisha mayai katika makundi kama ifuatavyo;
  • Rangi ya mayai
  • Rangi ya kiini cha yai(egg yolk colour), wengi wanapenda kiini cha rangi ya njano.
  • Ukubwa wa mayai
  • Aina ya mayai( mayai ya kienyeji yanapendwa zaidi kuliko ya kisasa)
8.      Fanya ukaguzi wa afya za kuku na kuwa tibu kila mara. Utaratibu unaopendekezwa ni kukagua afya asubuhi unapoamka na usiku unapoenda kulala. Angalia vinyeo ili kuona wanakunya kinyesi cha rangi gani(kinyesi ni kielelezo muhimu katika kutambua ugonjwa).
9.      Chunguza tabia za kuku ili kuona kama wanakula mayai au la . Ukiona kuku wameanza kula mayai fanya zoezi la kukata midomo mara moja kazi hufanywa na wataalamu , kwahiyo unashauriwa kumuona mtaalmu aliye jirani.
10.  Tunza kumbukumbu zote mradi  ili zikusaidie kufanya tathmini ya mradi unaoendesha.

UTAJIRI KATIKA MIRADI YA KUFUGA KUKU


UTAJIRI KATIKA MIRADI YA KUFUGA KUKU
Mradi wa kufuga kuku ni mradi ambao huleta faida kwa muda mfupi sana.
Ili upate faida kubwa ni vizuri ukawa na mradi ambao unaweza kuumudu kwa kuwa na mahitaji muhimu katika mradi wako.

MFANO, mtu anayetaka kufuga kuku tuseme 500 anatakiwa kuwa na vifaranga 550. Awe ana uwezo wa kuwalisha hao vifaranga na kuwapa tiba. Pia awe na uwezo wa kujenga banda bora.

 Baada ya hapo kinachotakiwa ni umakini wa kufuatilia mradi katika kipengele cha utoaji huduma kwa kuku hao. Katika kundi hilo la kuku 500, 50 wanatakiwa kuwa majogoo na 450 mitetea.
Katika hao mitetea 450 aslimia 75 wanatakiwa watage kila siku. Asilimia 75 ya 450 ni kuku 337. 

Mayai ya kuku hawa huuzwa kwa Tsh. 300@. Hivyo kila siku utapata Tsh 337 x 300 = Tsh. 100000.

Kama mtu anaweza kupata Tsh. 100000 kila siku kwa mwezi una uhakika angalau wa kuweka akiba ya Tsh. 100000 bila shida. Kama utaweka akiba ya fedha hiyo kila mwezi bila shida kwa mwaka utakuwa umeweka akiba ya shilingi milioni kumi na mbili.

Watu wengi wanaweza kufikiri hii ni nadharia ambayo haiwezekani, UKweli ni kuwa hiki kitu kinawezekana bila shida kabisa.

Ikiwa utahitahiji usaidizi njoo kwetu tukuelekeze namna unavyoweza kuondokana na umaskini usio wa lazima.

Kumbukeni ndugu wajasiriamali kwamba ukiamua ni kweli ndoto yako itatimia.

HISTORIA YA KUKU TANGIA KUUMBWA KWA DUNIA-KIBARA

HISTORIA YA KUKU (WAMETOKA WAPI?)

Kuku alitokana na jamii ya kuku-mwitu mwekundu wa Asia. Muda si muda, mwanadamu alitambua kwamba kuku anaweza kufugwa kwa urahisi. Inashangaza kwamba miaka 2,000 hivi iliyopita, Yesu Kristo alizungumzia jinsi kuku anavyokusanya vifaranga vyake na kuvilinda chini ya mabawa yake. (Mathayo 23:37; 26:34) Mfano huo unaonyesha kwamba kwa ujumla watu walimfahamu sana ndege huyo. Lakini kuku walianza kufugwa kwa wingi na mayai kutagwa kwa minajili ya biashara katika karne ya 19.
Leo nyama ya kuku inapendwa sana kuliko nyama ya ndege mwingine yeyote. Kuku hufugwa na mamilioni ya watu—hata wale wanaoishi mijini—kwa ajili ya chakula na biashara. Kwa kweli, ni wanyama wachache sana wa kufugwa wanaoweza kusitawi katika maeneo mbalimbali kama kuku. Nchi mbalimbali zimekuza kuku wa jamii fulani ambao wanaweza kukidhi mahitaji yao na kustahimili hali ya hewa ya sehemu hizo. Baadhi ya jamii hizo ni: kuku wa Australorp kutoka Australia; kuku ajulikanaye sana wa Leghorn, asili yake ni Mediterania lakini anapendwa sana nchini Marekani; kuku wa New Hampshire, kuku wa Plymouth Rock, kuku wa Rhode Island Red,na Wyandotte, kuku hao wanatoka Marekani; na Cornish, Orpington, na Sussex, wanatoka Uingereza.

Sayansi ya kisasa imefanya ufugaji wa kuku uwe mojawapo ya utendaji wenye faida sana katika kilimo. Nchini Marekani, wakulima hutumia mbinu bora za ulishaji na ufugaji. Wao pia hudhibiti magonjwa ya kuku kwa njia za kisayansi. Watu wengi hushutumu mbinu hizo za kisayansi za kuzalisha kuku wengi kuwa za ukatili. Lakini licha ya shutuma hiyo wakulima wangali wanabuni njia bora zaidi za kufuga ndege hao. Hivi sasa mtu mmoja tu anaweza kutunza kuku 25,000 hadi 50,000 akitumia mbinu za kisasa. Ndege hao huwa wamefikia uzani wa kutosha kuuzwa sokoni baada ya miezi mitatu tu.*

Chanzo cha Nyama

Waweza kuona nyama ya kuku ikiuzwa karibu kila mahali, iwe hotelini, mkahawani, au kwenye soko la nyama na vinywaji. Kwa kweli, mikahawa mingi ulimwenguni pote huuza hasa kuku. Jamii fulani hupika nyama ya kuku kunapokuwa na sherehe za pekee. Na katika baadhi ya nchi, kama vile India, mapishi mbalimbali ya kuvutia ya kuku yamebuniwa. Mapishi kama vile lal murgi,kuku aliyepikwa kwa pilipili-hoho; kurgi murgi, kuku aliyechanwa; na adrak murgi, kuku aliyepikwa kwa mchuzi wa tangawizi, huwa na ladha sana!

Mbona kuku wanapendwa sana? Kwanza, ni vyakula vichache tu vinavyoweza kutayarishwa kwa kutumia vikolezo mbalimbali. Wewe hupenda kuku aliyepikwaje? Je, unapenda kuku aliyekaangwa, aliyechomwa, aliyebanikwa, aliyepikwa kwa mvuke, au aliyechemshwa polepole? Ukitazama kitabu chochote cha mapishi huenda ukaona mapishi mengi sana ya kuku yanayokusudiwa kuboresha ladha ya kuku.
Kuku huuzwa kwa bei nafuu pia kwa sababu wanapatikana katika nchi nyingi. Wataalamu wa lishe hupendekeza nyama ya kuku, kwa sababu ina protini, vitamini, na madini ambayo ni muhimu kwa afya. Na bado, nyama ya kuku ina kalori chache, asidi-mafuta chache, na mafuta mengine.

Kulisha Nchi Zinazositawi

Bila shaka, nchi nyingine hazina bidhaa tele za kuku. Jambo hilo lapasa kufikiriwa kwa sababu ripoti ya tume maalumu ya Baraza la Sayansi ya Kilimo na Tekinolojia, ilisema hivi: “Idadi ya watu ulimwenguni inatarajiwa kuongezeka kufikia bilioni 7.7 mwaka wa 2020 . . . Hata hivyo, sehemu kubwa (asilimia 95) ya ongezeko hilo inatarajiwa kutukia katika nchi zinazositawi.” Taarifa hiyo inatisha zaidi unapofikiria kwamba tayari watu wapatao milioni 800 wana utapiamlo!

Hata hivyo, wataalamu wengi wanaona kwamba kuku wanaweza kutumiwa kulisha watu hao wenye njaa na wakulima wanaweza kupata riziki kwa kuuza kuku. Tatizo ni kwamba si rahisi kwa wakulima maskini kufuga kuku wengi sana. Jambo la kwanza ni kwamba katika nchi maskini kuku hufugwa hasa kwenye mashamba madogo vijijini, au katika vizimba vidogo. Na katika nchi hizo, kwa kawaida kuku hawatunzwi katika mazingira salama. Wakati wa mchana kuku huachiliwa ili wazurure-zurure ovyo na kutafuta chakula, kisha hurejea nyumbani usiku, nyakati nyingine wanalala mitini au katika vizimba vya mabati.

Si ajabu kwamba kuku wengi wanaotunzwa hivyo hufa—baadhi yao kutokana na ugonjwa hatari wa Newcastle na wengine huuawa na wanyama na wanadamu. Wakulima wengi hawana ujuzi wala uwezo wa kulisha kuku wao ifaavyo, hawawezi kuwatengenezea makao yafaayo, au kuwalinda na magonjwa. Ndiyo sababu miradi ya kuwaelimisha wakulima katika nchi zinazositawi imeanzishwa. Kwa mfano, Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo, hivi majuzi lilianzisha mradi wa miaka mitano wa “kuwasaidia wakazi maskini wa Afrika wanaoishi mashambani kupitia ufugaji wa kuku.”


Tungali twasubiri kuona matokeo ya jitihada hizo nzuri. Basi ni jambo lifaalo kwa wakazi wa nchi tajiri kutambua kwamba mlo wanaoona kuwa wa kawaida kwao kama vile kipande cha kuku yamkini ni mlo ghali sana kwa watu wengi duniani. Kwa watu hao, kula kuku ni kama ndoto tu.


                                                          WASILIANA NASI KWA; 


             

                                                                        0767-574 013
                                                              karolialex076@gmail.com